Sunday, May 6, 2012

Wastara apata...



Na Imelda Mtema
Msanii wa filamu ambaye amekuwa akiandamwa na mikasa tangu aolewe, Wastara Juma amepata pigo jipya baada ya hivi karibuni kuondokewa na bibi yake mzaa mama.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Wastara alisema bibi yake huyo alikuwa akiumwa na alilazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili lakini Ijumaa jioni akaaga dunia.
“Alikuwa mtu muhimu sana kwangu, amefariki wakati bado namhitaji ila sina jinsi zaidi ya kumuombea kwa Mungu ampumzishe mahali pema peponi,” alisema Wastara.
Aidha, Wastara aliwaomba Watanzania kuendelea kumchangia fedha ili kufanikisha matibabu ya mumewe Juma Kilowoko ‘Sajuki’ ambaye anasumbuliwa na tatizo la uvimbe tumboni.
Kwa rai hiyo, tunaomba tumchangie Sajuki fedha kupitia simu ya mkononi kwa kutuma kwenye Tigo Pesa namba 0713 666 113 au kwenye akaunti namba 050000003047 katika Benki ya Akiba Commercial yenye jina la Wastara Juma Issa.






Na Sifael Paul
UKWELI ni kwamba mastaa wawili wakubwa wa filamu za Kibongo ambao ni wanandoa, Wastara Juma na Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ hawajawahi kufurahia maisha ya ndoa yao tangu walipooana Juni 6, 2009 kufuatia kuandamwa na mikosi kila kukicha, Amani lina ripoti kamili.
Katika maisha yao ya ndoa, wawili hao wamekuwa wakipokezana mateso huku likiibuka jipya la kuwatoa machozi mara kwa mara na sasa Sajuki ndiye anayewaliza watu kufuatia kusumbuliwa na maradhi ya uvimbe tumboni.
Ili kushibisha hoja kuwa wawili hao hawajawahi kuwa na furaha, shuka na data zifuatazo;
MACHI 12, 2009
Wakiwa wachumba, Wastara na Sajuki walipata ajali mbaya ya ‘bodaboda’ maeneo ya Tabata, Dar es Salaam ambapo mwanadada huyo alikatika mguu, hapo ndipo furaha ya wawili hao ilipoanza kutoweka.
MWAKA 2010
Baada ya kufunga ndoa, miezi kumi ya mwaka 2010, maisha hayakuwa mazuri kwani Wastara aliishi bila mguu mmoja hadi alipowekewa wa bandia Nairobi, Kenya ukiwa na gharama ya Sh. milioni 7.
AGOSTI 29, 2011
Wastara alikimbizwa hospitalini na kulazwa baada ya kubainika kuwa alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa nimonia.
Hata hivyo, baadaye ilibainika kuwa alikuwa mjamzito lakini alificha kwa kuwa aliogopa lolote linaweza kutokea kwani alikuwa akisemwa juu ya kutopata mtoto, hivyo kupoteza raha ya ndoa yao.
OKTOBA 29, 2011
Machozi mengine! Sajuki naye aliripotiwa kuwa hoi kitandani akisumbuliwa na uvimbe tumboni ambapo zilihitajika Sh. milioni 6 kwa ajili ya matibabu hivyo kupoteza kabisa furaha ya wanandoa hao.
MACHI 7, 2012
Wakati Sajuki bado mgonjwa akijiandaa kwenda kutibiwa nchini India, ndoa yao ilipata uzao wa kwanza, lakini hawakuweza kufurahia kwa sababu jamaa huyo yuko hoi.
APRILI 2, 2012
Sajuki alirejea kutoka katika Hospitali ya Apollo nchini India alikopeleka vipimo vya afya yake na kupata matibabu ambapo alisema alikuwa amepata nafuu kidogo kabla ya hivi karibuni hali kuwa mbaya zaidi na kuibua vilio upya ambapo kila Mtanzania anaombwa kutoa mchango wake wa hali na mali ili arudishwe India.
MCHANGO
Ili kumchangia Sajuki akatibiwe, tuma Tigo Pesa kwenda namba 0713 666 113 au akaunti ya Benki ya Akiba Commercial namba 050000003047 yenye jina la Wastara Juma Issa.



Na Imelda Mtema
MWIGIZAJI wa filamu za Kibongo,  Aunt Ezekiel na mwimbaji wa Taarab, Aisha Ramadhan ‘Isha Mashauzi’ wamezua timbwili kisa kikidaiwa kuwa ni mwanaume, Ijumaa Wikienda lina kila kitu.
Kwa mujibu wa shuhuda wetu, tukio hilo lilitokea Ijumaa, saa 10 alfajiri katika pub inayomilikiwa na Aunty iliyopo Mwananyamala Gereji, jijini Dar baada ya Mashauzi kufika akiwa na wenzake sambamba na mwanaume aliyefahamika kwa jina moja la Jumanne.
“Walipofika walitaka kuhudumiwa, Aunt akakataa kwa madai kuwa tayari alishafunga,” kilisema chanzo chetu na kuongeza kuwa visa kati ya wawili hao vilianza siku kadhaa zilizopita baada ya Isha kumtuhumu Aunt kuwa anatoka na Jumanne.
Baada ya kunyimwa huduma, Isha alianza kurusha vijembe kwa Aunt, naye akajibu mapigo kwa kuanza kumponda Jumanne kuwa aache kujisifu kuwa anatoka naye kimapenzi.
Katika timbwili hilo, Aunt alimsukuma Jumanne aliyeangukia kwenye viti, hali iliyomfedhehesha sana, akampiga marufuku ya kufika kwenye pub yake.
Jitihada za kuwapata wahusika kuzungumzia sakata hilo hazikuweza kufanikiwa.

Miss Jokate



Na Mwandishi wetu
Upepo wa habari za chini ya kapeti umemgeukia Miss Jokate Mwegelo, mrembo namba 2 kwenye Shindano la Miss Tanzania 2006, nyuma ya mshindi Wema Sepetu aliyevaa taji kuwa msichana huyo havumi lakini yumo kwenye msafara wa matukio ya kimapenzi.
Mitandao mingi ya kijamii hivi karibuni imemfumua Jokate kuwa ni simba mwenda kimya mawindoni kufuatia msanii wa muziki wa kizazi kipya, Naseeb Abdul ‘Diamond’ kuutangazia umma kuwa anatoka na mrembo huyo.
Siku chache zilizopita, Wema Sepetu ambaye alikuwa mchumba wa Diamond kabla hajabwaga manyanga alilalama kwenye vyombo vya habari kuwa Jokate ameingilia penzi lake kwa msanii huyo, tuhuma ambazo miss huyo namba 2 aliziruka kwa kusema anasingiziwa.
“Si alikuwa anakanusha, sasa yako wapi?” Jane Swai, mchangiaji wa blogu (jina kapuni) alihoji wakati akitoa maoni yake kuhusu habari ya Diamond kutangaza rasmi kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na msichana huyo mwenye kidoti cheusi usoni na kwamba haoni mwingine wa kumpa penzi lake.
Wakati Jokate akisakamwa kwenye mitandao, Uswahilini nako hali si shwari ambapo dodoso nyingi zisizokuwa na uthibitisho wa kutosha zimekuwa zikitolewa kwamba mwanadada huyo kabla ‘kudeti’ na Diamond ameshatoka na msururu wa wanaume wengine.
Wachache kati ya wanaume wanaotajwa mitaani na ambao Jokate amekuwa akikanusha vikali kutoka nao kama alivyokuwa akikana kwa Diamond ni Hashim Thabeet, Hamis Mwinjuma ‘Mwana FA’ na Ambwene Yesaya ‘AY.’
“Jokate ni msiri lakini ameshatoka na (anawataja mastaa hao waliopo  paragrafu ya juu) na hata …(anamtaja kijana mmoja ambaye baba yake ana wadhifa mkubwa serikalini) naye ametembea naye, hata mzee… (anamtaja mfanyabiashara maarufu nchini) ameshapita, ni vema awe wazi kuna siku ataumbuka,” alidai Julieth John, mwanamitindo anayefanya shughuli zake jijini Dar es Salaam.
Siku chache tangu Diamond aanike kile kilichokuwa kikifichwa kati yake na miss huyo namba 2, mchumba wake wa zamani, Wema alitoa kauli hii: “Niliposema watu waliniona mjinga lakini sasa Jokate kaumbuka.”
 Jokate kwa upande wake amekuwa kimya.

GONJWA LA AISHA MADINDA

GONJWA LA AISHA MADINDA LAMTESA JANETH ISNIKA


Janeth Isnika.
Na Musa Mateja
MWIMBAJI katika safu ya wanawake wa Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta International’, Janeth Isnika, yu- hoi kitandani akiuguza ugonjwa wa miguu kama uliokuwa ukimtesa aliyewahi kuwa Mnenguaji wa Extra Bongo, Aisha Ramadhani Mbegu ‘Aisha Madinda’.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni Janeth alisema ana muda wa takribani mwaka mmoja anauguza magoti yake na kila anapopata nafuu maumivu hurudi upya kama ilivyokuwa kwa Aisha.
“Kusema kweli miguu hii inanitesa sana, napata tabu sana, nalala kwa mateso makubwa hasa kipindi cha baridi kali, mashabiki wangu waniombee tu kwani wakati mwingine nafikia hatua ya kukufuru,” alisema Janeth.
Kufuatia hali hiyo, muimbaji huyo ambaye pia ni tishio kwa kunengua ana muda mrefu hajapanda jukwaani hivyo kuwafanya mashabiki wake kukosa manjonjo yake. Gazeti hili linamuombea apone haraka ili aendelee na kazi yake ya kuiburudisha jamii.

MASTAA WAANGUA VILIO


MASTAA WAANGUA VILIO UPYA KIFO CHA KANUMBA



Davina akifuta machozi.

Recho akiangua kilio.
Odama akiwa na simanzi.
Uwoya (kushoto) na Shilole wakiwa na majonzi.
Gladness Mallya na Erick Evarist
BAADHI ya mastaa wa filamu Bongo juzikati walijikuta wakiangua vilio kwenye Ukumbi wa Business Park, Kijitonyama jijini Dar baada ya kusikia wimbo maalum wa kumuenzi marehemu Steven Kanumba.
Ishu hiyo ilitokea juzikati kwenye utambulisho wa wanamuziki wapya waliojiunga na Bendi ya Mashujaa Musica ambapo kabla ya wimbo huo, mastaa hao walikuwa wamekaa pamoja wakijiachia kwa raha zao.
Wakati shoo ikiendelea, ulifika wakati Steve Nyerere akaitwa jukwaani kwa ajili ya kuungana na wanamuziki hao kuimba.
Akiwa jukwaani, Steve alitumbuiza kisha aliwataka watu wote wasimame kwa ajili ya kumkumbuka Kanumba, wimbo maalum wa kumuenzi marehemu ulipopigwa ndipo mastaa walipoanza kububujikwa na machozi.
Mastaa walioshindwa kujizuia kuangua vilio ni Irene Uwoya, Halima Yahaya ‘Davina’, Jennifer Kihaka ‘Odama’, Rachel Haule ‘Recho’ na mpenzi wake ambaye ni mpigapicha wa Kampuni ya RJ, Saguda George.
Achilia mbali mastaa hao, pia mashabiki waliokuwa wamefurika ukumbini hapo walipoteza furaha na kuanza kuomboleza upya kifo cha Kanumba na kuifanya burudani iignie mdudu.

The Old Lady is back: Juventus is Italy's best again as it roars to Scudetto glory

The Bianconeri have returned to the top of the Italian game, and their magnificent 37-match unbeaten run proves they are deserving champions

Juventus celebrating
Getty Images
The Old Lady is back. Six years after the shame, the conjecture, the recriminations and the introspection, Juventus is champion of Italy once more. And boy, how it's taken Serie A by storm in achieving that. Everybody knew that this day would come, but it was almost as though the Bianconeri had to make an extra statement in making it happen, and tonight’s victory over Cagliari not only returns the Scudetto to Turin, but it also leaves Juve within 90 minutes of a unique 38-game unbeaten season. This isn’t just a title win, it’s a declaration.
Not only has Juve yet to be bowed, it have gone about destroying most of the peninsula’s top-flight clubs. While the scorelines have not always reflected the club's dominance, it has been about as impressive as any Italian side in living memory.
TOP MARKS | Juve's leading scorers
Alessandro Matri
Mirko Vucinic
Claudio Marchisio
Arturo Vidal
Simone Pepe
Fabio Quagliarella
Andrea Pirlo
10
9
9
7
6
4
3
From their high pressing game and their near-faultless midfield base to an almost impregnable defence, the Bianconeri have had pretty much every facet covered. Even their poor conversion rate has been practically forgotten in the last 10 matches, with 26 goals helping them negotiate the potentially difficult run in like a batter smashing home run after home run in a World Series decider.
Had their shooting boots fit so snuggly during the first three quarters of the season, the title could have been won two months ago, such has been their clear superiority over the opposition. But it is not only a glorious achievement, to the majority of calcio fans it is also a great surprise.
At the beginning of the season the main question mark hanging over Juve was in relation to its readiness to compete for a Champions League spot. With back-to-back seventh place finishes and the reduction of Italian representation for the main event in 2012-13, there were doubts among many as to whether the Bianconeri had what it would take to make a four-place leap in the standings.
But from early in the piece, it was clear that Antonio Conte’s outfit was a very different animal to the one steered off course by Ciro Ferrara, Alberto Zaccheroni and Luigi Del Neri over the previous 24 months. Instead of the fractured build-up play, there was unprecedented fluency. Where there had been pressure on their back-line, there was now a switch of emphasis to ensure that the defence was tested as rarely as possible.
This was a whole new Juve, with a new stadium, a new coach and a brand new philosophy defining its new era. And while it struggled to make its superiority count at times, there was never an inability to assert authority.
It may not be the best Juventus ever, with many great versions of the past staking a claim for that crown, but that is not important right now. The fact is that the Bianconeri are back. Champions again, and convincingly so - however much Milan coach Massimilano Allegri argues otherwise, in relation to Sulley Muntari's phantom goal back in February. Rarely has a team’s supremacy been so unquestionable.

ODAMA

ODAMA: NAMALIZIA ‘BATA’ KWANZA, NDOA BAADAYE

 Jennifer Kyaka ‘Odama’.
Na Gladness Mallya
MWANADADA anayefanya vizuri kunako gemu la filamu Bongo, Jennifer Kyaka ‘Odama’ amefunguka kuwa kwa sasa hawezi kukurupukia kuolewa hadi atosheke kula starehe ‘bata’ kwa kujinafasi.
Akichonga na paparazi wetu, Odama alisema amefikia hatua ya kusema hivyo kwa kuwa, anajua ndoa inahitaji utulivu kiasi kwamba akiolewa haraka huku akiwa bado ana hamu ya kujiachia anaweza kutibua ndoa.
“Ukiwa ndani ya ndoa utakuwa unabanwabanwa na mwanaume, huwezi kula bata kama unavyoweza kula ukiwa singo kwa hiyo bora nimalizie kabisa nikiingia huko niwe nimetosheka,” alisema Odama.
Akaongeza kuwa, wengi ambao ndoa zao hazidumu wamepapatikia kuolewa ila yeye ataolewa akiwa na miaka 35 na atazaa mtoto mmoja tu.

SIMBA SC NGRIIIIIIII!


Na Khatimu Naheka
LLOYD Nchunga jana alishindwa kuvumilia na kuamua kukimbia uwanjani baada ya timu yake kufungwa bao la nne, wakati Yanga ilipopokea kipigo cha mbwa mwizi cha mabao 5-0 kutoka kwa wapinzani wao, Simba.
Mwenyekiti huyo ambaye hivi karibuni alijikuta katika wakati mgumu, baada ya wazee wa klabu yake kutaka kuichukua timu mikononi mwake, alishuhudia mvua ya mabao kutoka kwa mabingwa, Simba, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar na kuzidi kuwa katika hali ngumu zaidi.
Katika mchezo huo, Simba walianza kupata bao dakika ya kwanza tu ya mchezo kupitia kwa Emmanuel Okwi aliyeunganisha vizuri pasi ya Felix Sunzu baada ya Nurdin Bakari kupoteza mpira karibu na lango la Yanga.
Baada ya bao hilo, Yanga walifanya mashambulizi kadhaa katika dakika ya tisa na 11 huku shuti moja lililopigwa na Athuman Idd ‘Chuji’ likigonga mwamba na kurejea dimbani kabla Hamis Kiiza kupiga tena na safari hii mlinda mlango Juma Kaseja akiucheza mpira na baadaye kuokolewa na mabeki wake.
Kipindi cha kwanza kiliisha kwa Simba kuendelea kuongoza kwa bao 1-0 lakini kipindi cha pili ndicho kilichopeleka simanzi kubwa Jangwani baada ya kushuhudia kipa Said Mohammed aliyechukua nafasi ya Yaw Berko, akiokota mipira minne langoni mwake.
Aibu ya Yanga ilianzia dakika ya 53, baada ya Felix Sunzu, kupiga penalti kwa ufundi akiandika bao la pili. Penalti hiyo ilitokana na Okwi kuchezewa faulo katika eneo la hatari.
Dakika ya 62, Okwi alifanya tena kazi ya ziada, alipomtoka beki mkongwe, Shadrack Nsajigwa na kufunga bao safi lililowaacha wachezaji wa Yanga wakiwa wameshika viuno kwa huzuni.
Huku Jangwani wakiendelea kujiuliza, Simba walipata penalti nyingine katika dakika ya 66 baada ya Okwi kufanyiwa faulo tena ndani ya eneo la hatari na kipa, Mohammed. Juma Kaseja ndiye aliyepiga penalti hiyo na kuiandikia Simba bao la nne.
Katika hali ya kushangaza, Simba walipata penalti ya tatu dakika ya 71 iliyotokana na beki, Athuman Idd ‘Chuji’ kumfanyia faulo Okwi ndani ya eneo la hatari. Patrick Mafisango alipiga penalti hiyo na kufikisha bao lake la 11 kwenye Ligi Kuu ya Bara msimu huu.
Katika tukio la kusikitisha, mashabiki wawili wa Yanga walizimia na kubebwa na watu wa Msalaba Mwekundu, baada ya Mafisango kufunga bao la tano huku Kocha Msaidizi wa timu hiyo, Fred Felix Minziro, akigoma kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu mchezo huo.
Naye Kocha Mkuu wa Simba, Milovan Cirkovic, amesema baada ya kufanikiwa kutwaa ubingwa, kwa sasa wanachokiangalia ni kufanya vizuri kwenye michuano ya kimataifa.
Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza Yanga ilifanikiwa kuichapa Simba bao 1-0.
Katika matokeo mengine, licha ya Villa Squad kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Mlandizi, Pwani, ilijikuta ikishuka daraja na kuungana na Polisi Dodoma pamoja na Moro United.
Kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, JKT Oljoro ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Polisi, wakati huko Mkwakwani, Tanga, Toto ilipata kipigo kama hicho kutoka kwa Coastal Union na kunusurika kushuka daraja kutokana na kuwa na uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa licha ya kuwa na pointi 26 sawa na Villa.
Mtibwa Sugar iliendeleza ubabe wake kwa kuifunga Moro United bao 1-0 kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, Azam ikiishinda Kagera mabao 2-1, Chamazi, Dar na African Lyon ikiibamiza JKT Ruvu mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro.

Arsenal reveal home kit for 2012/13 season


Arsenal Football Club is proud to unveil its new home kit for the 2012/2013 season.

Available to pre-order from Club stores and online at www.arsenaldirect.com, the playing kit features a blue hoop detail inspired by the home kit socks worn in the 1930s under legendary manager Herbert Chapman.

As is traditional with the north London club, the world renowned red and white is the main colour way in the shirt, with a block red body and white sleeves.
Click here for pictures of the new kit

Further details in the shirt include the outer back neck graphic which references the WM formation that Chapman pioneered so successfully, along with the inner back graphic which reads “Victoria, Concordia, Crescit” – the Club’s long-held motto since 1948 which translates as Victory through Harmony*.

The origins of the blue (obsidian) design features lie in Chapman’s innovative approach to the game. Arsenal manager between 1925 and 1934, his guidance took the Club to three league titles and an FA cup victory during that time.

Chapman was a modernising tactician, advocated the use of numbered shirts and white balls, and also made significant changes to the Club’s kit for the 1933/34 season. In that year white sleeves were added to the previously all-red shirt and blue hoops were also introduced to the socks. Chapman’s rationale for these innovations was he wanted to maximise player visibility, making it easier for his players to pick each other out on the field of play.

Arsenal’s Theo Walcott commented: “The players always get excited about trying on kits for the first time, and this one doesn’t disappoint. Arsenal is a club with an incredible history and to see this recognised in such a classy and modern kit is brilliant.”

The shirt’s crest reverts back to Arsenal’s primary design, having sported a unique 125th anniversary version for the 2011/12 season.

The kit is available for pre-order from Monday, May 7 and will be available in stores from June 7. Anyone ordering the kit from an Arsenal retail channel will receive a limited edition collector’s box and back pack (while stocks last).

There is also the chance to win a Citroen DS3** featured in the exclusive kit shoot video which can be seen by clicking the image above. Supporters can also see the car in the Armoury Store from Tuesday, May 8. Adult shirts are priced from £45 with youth shirts from £35, available for pre-order at www.arsenaldirect.com.

Messi breaks record for most goals scored in a single European league season

The Argentine's record-breaking year is showing no signs of abating after he broke Dudu Georgescu's feat of 47 strikes in a single league campaign on the continent.

Lionel Messi
David Ramos
Lionel Messi has now scored the most goals in a single European league season after netting four times in Barcelona's 4-0 victory over Espanyol on Saturday.

The prolific forward broke Dudu Georgescu's record of 47 goals for Dinamo Bucharest in the 1976-77 campaign when he put the Blaugrana 2-0 up during the Catalan derby at Camp Nou.

Messi is now on 50 league goals for the season, having followed up his pair of strikes with two more on the night and securing his eighth hat trick of the campaign in the process.

The record is just one of several in what has been a memorable season for the Argentine, beginning with his five goals against Bayer Leverkusen in the Champions League to earn him the distinction of being the competition's first player to score five in a single match.